Tunamshukuru kwa dhati kabisa Allah sub-hanahu wa ta'ala kwa kutuwezesha kufika tulipo fika katika mwezi huu wa Ramadhani, pia rehma na amani zimshukie Mtume, pamoja watu wake na sahaba zake na wale wote wenye kufuata mwenendo wake mpaka siku ya qiyama. Na tunashuhudia kwamba hapana Mola anayestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah na Muhammad ni mja na Mtume wake.
Mwezi mtukufu wa Ramadhani ndio umefikia ukingoni, wengi ni wenye huzuni kwani ingawa ni mwezi mmoja tu, wamejenga mazoea makubwa ya kufanya mambo mbali mbali ambayo hatuyapati katika miezi mingine, mikusanyiko ya pamoja katika milo ya iftaar, misikiti kujaa, itikafu, qiyamul layl na du’a za kuomba maghfira kama vile
soma zaidi



0 comments