Friday, October 12, 2012

UPDATE KATIKA KURASA ZA SIB KUCHELEWA

Update katika kurasa za blog ya michezo ya Sports In Bongo (www.aboodmsuni.blogspot.com) 'SIB' iliyopo chini ya usimamizi wa Aboodmsuni Network zitakuwa zinachelewa kutokana na kuharibika kwa 'Motherbody' ya laptop iliyokuwa inatumika katika kuendesha shughuli za blog.

Kuharibika kwa machine hiyo kulipeleka Aboodmsuni Network kutumia simu katika uendeshaji wa blog katika wiki mbili zilizopita ambapo kwasasa inawajia vigumu kutokana na 'platform' ya blogger kuboreshwa na kupelekea simu tunayo itumia kushindwa kufanya kazi ya kuupdate.

Aboodmsuni Network inafanya kila liwezekano kurejea katika hali ya kawaida katika huduma yake ya uwendeshaji wa blog ya Sports In Bongo 'SIB'.

Kwa sasa update za kurasa za SIB, hususani ile ya Msimamo wa ligi utakuwa unafanywa katika wikidays saa za kazi, ambapo blogger wetu Abdallah Sulayman 'Msuni' atapata fursa ya kutumia komputer za college pale anapo pata mda, wa kufanya hivyo.

0 comments